KAGONGWA WAKABIDHIWA GARI LA WAGONJWA NA MBUNGE KISHIMBA, AOMBA TIBA KWA WANANCHI ITOLEWE BURE KAMA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 15 March 2024

KAGONGWA WAKABIDHIWA GARI LA WAGONJWA NA MBUNGE KISHIMBA, AOMBA TIBA KWA WANANCHI ITOLEWE BURE KAMA ELIMU YA MSINGI NA SEKONDARI

Kituo cha afya Kagongwa kinachohudumia wananchi takribani 60,000 wa Kata za Kagongwa, Mondo na Isagehe kwa mujibu wa sensa ya watu na makazi  ya mwaka 2022 kimepokea gari la kubebea wagonjwa [Ambulance] kwa ajili ya wagonjwa kupata huduma.



NA NEEMA NKUMBI-HUHESO DIGITAL


Gari hilo limekabidhiwa March 14, 2024 na Mbunge wa Jimbo la Kahama mji Jumanne Kishimba katika hafla ya makabidhiano yaliyofanyika Kata ya Kagongwa Manispaa ya Kahama Mkoani Shinyanga, Kishimba amesema kuwa gari hilo limekabidhiwa ili kuokoa uhai wa wananchi hivyo hawana budi kulitunza.


Wananchi wa Kata ya Kagongwa wamesema kuwa kupatikana kwa gari hilo kutasaidia kuokoa uhai wa wagonjwa hasa wanawake na watoto wanao kabiliwa na changamoto nyingi za kiafya.


''kupatikana kwa ambulance hii kutatusaidia sisi akina mama hata tunapokwenda kujifungua kwani tulikuwa tunapata shida mpaka tuite bodaboda lakini mama Samia Suluhu Hasan ametusaidia sana'' amesema Zena Nasoro


Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Hospitali ya Wilaya ya Kahama Dr Fredrick Malunde licha ya kupokea gari hilo anatambua uwepo wa changamoto ya upungufu wa watumishi kwenye kituo hicho atahakikisha wanaongezeka pindi serikali itakapotoa ajira.


''Natambua kwamba kituo changu cha afya kagongwa kina watumishi 26 hivyo tutakapopata ajira mpya tutaongeza madaktari na watumishi wengine ili kupunguza mzigo katika hospitali ya wilaya kahama, pia tutapunguza vifo vya akina mama na watoto chini ya miaka mitano [5] katika eneo hili'' amesema Dr malunde


Mara baada ya kukabidhi gari hilo mbunge Jumanne Kishimba  amesema changamoto ya matibabu bado ni kubwa ataendelea kumwomba Mheshimiwa Rais Samia kupitia bunge kufanya matibabu kuwa bure kama ilivyo elimu bure kwa sasa.


''Tunaendelea kuiomba serikali katika swala la matibabu ilitazame kwa jicho la upana sana kuwasamehe watoto shule na matibabu pia iwe bure kwa sababu ni kitu cha lazima'' amesema Mbunge Kishimba.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso