MAREKANI YAPITISHA MUSWADA KUPIGA MARUFUKU TIKTOK - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 14 March 2024

MAREKANI YAPITISHA MUSWADA KUPIGA MARUFUKU TIKTOK


Wabunge wa Baraza la Wawakilishi nchini Marekani wamepitisha muswada wa sheria wa kupiga marufuku mtandao wa TikTok nchini humo, iwapo wamiliki wake watakataa kuuza sehemu ya udhibiti wake kwa Marekani ndani ya kipindi cha miezi sita.





Uamuzi huo umepitishwa leo na wabunge wa vyama vyote vya Republican na Democratic, sasa unasubiri uamuzi wa Kampuni ya ByteDance ya China inayomiliki mtandao wa TikTok kukidhi matakwa ya Baraza na ikishindikana muswada utapelekwa kwenye Seneti kutungiwa sheria na atapelekewa Rais Joe Biden kutia saini kuwa sheria kamili.


Baraza la Wawakilishi lina wajumbe 435, wengi wanatoka chama cha Republican ikifuatiwa na Democratic, huku Seneti yenye jumla ya wajumbe 100, wengi wanatoka chama cha Democratic ikifuatiwa na Republican.


Seneti na Baraza la Wawakilishi ndio wanaunda Bunge la Marekani linaloitwa ‘Congress’ lenye majukumu kama vile kutunga sheria, kutangaza vita, kumshitaki Rais na kupitisha wateule wa Rais.


Uamuzi wa kuifunga TikTok utaiondolea Marekani mapato ya matangazo yanayokadiriwa kufikia Dola 8.66 bilioni ikilinganishwa na mapato ya Dola 1 bilioni ya mwaka 2020.


Hata hivyo, uamuzi huo umepitishwa wakati tayari Rais Joe Biden amefanya utambulisho wake wa kugombea tena urais kwa njia ya TikTok, huku baadhi ya wanasiasa wakiwamo wa chama chake cha Democratic na wale wa Republican wakimshutumu kutumia mtandao huo wa China.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso