JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA MTOTO WA KAKA YAKE - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 14 March 2024

JELA MIAKA 30 KWA KUBAKA MTOTO WA KAKA YAKE


Mahakama ya Wilaya ya Mufindi, imemhukumu kifungo cha miaka 30 jela, Rodick Msilwa (20) baada ya kumpata na hatia ya kumbaka mtoto wa kaka yake mwenye umri wa miaka 10.
Hukumu ya kesi hiyo namba 1,392 ya mwaka 2024 imetolewa jana Machi 13, 2024 katika Mahakama ya Wilaya ya Mufindi mkoani Iringa na Hakimu Mkazi Mfawidhi, Benedict Nkomola.





Akisoma shtaka hilo, Hakimu Nkomola amesema tukio hilo limetokea Desemba 12, 2023 mchana huko Kijiji cha Luholofu, Kata ya Mgololo, baada ya mtoto huyo kutumwa shambani na mama yake kwenda kuchukua maharage, lakini wakati anarudi ndipo alikutana na mshtakiwa na kubakwa.


"Alitumwa shambani na mama yake akiwa na mdogo wake wakiwa shambani waliitwa na mshtakiwa ambaye ni baba yake mdogo.Alimchukulia na kumpeleka kwenye nyasi kisha akamlaza chini na akamvua nguo yake ya ndani akiwa amemziba mdomo ili asiweze kupiga kelele na kumbaka na baada ya kumaliza alimuahidi atampa Sh1,000 pamoja na pipi." ameeleza hakimu huyo.


Baada ya mshtakiwa kusomewa hati ya shtaka lake, alikana kutenda kosa hilo ndipo Mahakama ikaalika upande wa mashtaka kwa ajili ya kuthibitisha shtaka hilo.


Hakimu huyo amesema upande wa mashtaka ulithibitisha shtaka hilo bila kuacha shaka kwa kuleta mashahidi sita pamoja na kielelezo kimoja cha PF3 cha ofisa tabibu, ambacho kilionyesha mtoto huyo aliingiliwa sehemu zake za siri kwa sababu alikuwa na michubuko.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso