MTUHUMIWA WA UVAMIZI WA KANISA GEITA AMHOJI PADRI - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday 29 August 2023

MTUHUMIWA WA UVAMIZI WA KANISA GEITA AMHOJI PADRI



Mshtakiwa Elpidius Edward mkazi wa Mtaa wa Katundu Wilaya ya Geita anayedaiwa kuvamia Kanisa Kuu la Kiaskofu jimbo Katoliki Geita na kufanya uharibifu uliosabisha hasara ya Sh48.2 milioni amemtaka shahidi wa tano katika kesi hiyo kuieleza Mahakama kwanini hakupeleka mahakamani hapo ushahidi wa kamera za CCTV alizomkuta akiharibu.


Mshtakiwa huyo ambaye hana wakili alianza kumuuliza maswali shahidi huyo wa tano ambaye ni Padri Charles Kato wa kanisa katoliki jimbo la Geita mara baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake aliokuwa akieleza Mahakama namna alivyomkuta mshatakiwa akifanya uharibifu ndani ya kanisa hilo.


Mshatakiwa huyo alihoji kama alimkuta akivunja CCTV Kamera kwanini hakuipeleka mahakamani kwa kuwa ndio ushahidi wenye uhalisia kuliko kuja mwenyewe kuieleza Mahakama.


Akijibu swali hilo Shahidi Kato amedai asingeweza kuleta ushahidi wa CCTV kamera kwakuwa tayari mshtakiwa aliharibu mfumo wa CCTV kabla ya kuifikia kamera.


Mshtakiwa huyo pia alitaka kujua mtu sahihi aliyefungua mlango wa kanisa kutokana na shahidi aliyetangulia kudai siku ya tukio yeye ndie aliyekuja na funguo na kufungua lango kuu la kanisa kisha walinzi kuingia na kumdhibiti na leo shahidi huyo anaeleza yeye ndie aliyefungua kanisa hilo.


Akijibu swali hilo Shahidi Kato amedai kuwa yeye alipita kwenye mlango wa ‘Sakristia’ (mlango wa pembeni) ulipo mtambo wa CCTV camera akiwa na walinzi wanne na ndipo alipomkuta akiharibu mfumo wa kamera za kanisa hilo.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso