SERIKALI YAKATA RUFAA DHIDI YA BOSI WA GOLDEN TULIP - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 18 July 2022

SERIKALI YAKATA RUFAA DHIDI YA BOSI WA GOLDEN TULIP



Baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kumfutia kesi ya uhujumu uchumi mfanyabiashara Jitesh Jayantilal Ladwa, Serikali imemkatia rufaa Mahakama Kuu ikitaka kesi hiyo irejeshwe.


Jitesh alipandishwa kizimbani kwa kesi ya uhujumu uchumi, akituhumiwa kughushi na kujihamishia hisa za wanahisa wenzake katika Kampuni ya Indian Ocean Hotels Limited, inayomiliki hoteli za Golden Tulip.


Hata hivyo, Mahakama ya Kisutu ilimfutia kesi hiyo baada ya kukubaliana na hoja za pingamizi za wakili wake, Jeremiah Mtobesya kuwa Mahakama hiyo haikuwa na mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo ya jinai.


Baada ya uamuzi huo, Serikali imekata rufaa Mahakama Kuu nayo ikiipinga Mahakama ya Kisutu kuwa haina mamlaka ya kutoa uamuzi kama huo wala kusikiliza pingamizi.


Wakili wa Serikali Mwandamizi, Ester Martin alilieleza Mwananchi hivi karibuni kuwa Serikali imekata rufaa kupinga uamuzi mahakamani kumfutia mashtaka Jitesh huku ikiwa na sababu tatu.


Alidai kuwa bado wanasisitiza Mahakama ya Kisutu ilikosea kutoa uamuzi huo kwa kuwa haina mamlaka ya kuamua wala kusikiliza hoja yoyote kutoka kwa mshtakiwa.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso