BABA NA MTOTO WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KIFO-MARA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 27 May 2022

BABA NA MTOTO WAHUKUMIWA KUNYONGWA HADI KIFO-MARA


Mahakamani Kuu Kanda ya Musoma kupitia Mahakama ya Wilaya Tarime Mkoani Mara imewahukumu baba na mtoto wake wa Kijiji cha Genkuru kunyongwa hadi kufa baada ya kupatikana na hatia ya mauaji.


Waliohukumiwa ni Matinde Keranganyi (baba) na Mwita Matinde (mtoto) ambao walishtakiwa kwa kumpiga mawe, kumkata mapanga na kumchoma mkuki Chacha Nyamhaga, wakigombea ardhi.


Hukumu hiyo ilisomwa na Msajili wa Mahakama Kuu Kanda ya Musoma, Frank Moshi.


Awali, Mwanasheria wa Serikali, Yese Temba, alidai kuwa washtakiwa Mei 25, 2019 kwa makusudi wakiwa na silaha za jadi walimvamia Nyamhanga akiwa shambani kwake kumshambulia kwa kumpiga mawe na kuanguka chini na kisha kumchoma mkuki na kumkata mapanga kichwani hali iliyosababisha kifo chake.


Chanzo cha mauaji hayo kimedaiwa kuwa ni mgogoro wa ardhi kati ya marehemu na washtakiwa hao.


Upande wa mashtaka ukiongozwa na Mwanasheria wa Serikali Temba ulileta mashahidi saba vikiwamo vielelezo na PF3, mganga aliyefanya uchunguzi wa mwili wa marehemu na upande wa utetezi ulileta mashahidi wanne.


Msajili wa Mhakama Kuu, Moshi alisema Mahakama imeridhika na ushahidi uliotolewa na upande wa mashtaka bila kuwapo shaka lolote.

CHANZO:LANGO LA HABARI

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso