NA NEEMA NKUMBI -HUHESO DIGITAL KAHAMA
Mjasiriamali ambaye pia ni Mwenyekiti wa bodaboda mkoa wa Shinyanga Idsam Swalehe Mapande, leo Julai 2, 2025, amerejesha fomu ya kuomba ridhaa ya kugombea udiwani kata ya Kahama Mjini kupitia tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)
Fomu hiyo imepokelewa na katibu wa CCM kata ya Kahama Mjini Charles Sazia Nkwabi, ikiwa leo ndio tamati ya kuchukua na kurejesha fomu za watia nia wa nafasi mbalimbali za uwakilishi wa wananchi kupitia CCM, kuelekea uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani.
No comments:
Post a Comment