UCHAGUZI WA RAIS KUFANYIKA MWEZI HUU - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 7 March 2024

UCHAGUZI WA RAIS KUFANYIKA MWEZI HUU


WAPIGA kura nchini Senegal wataamua hatma ya rais wao ajaye mnamo Machi 24, Rais Macky Sall ametangaza leo.


Baraza la Katiba lilitoa uamuzi kwamba itakuwa kinyume na katiba kufanya uchaguzi wa urais baada ya Aprili 2, tarehe inayoashiria mwisho wa muhula wa sasa wa rais.


Baraza hilo liliamua kwamba uchaguzi huo ufanyike haraka iwezekanavyo, huku wakipinga mapendekezo ya mazungumzo ya kitaifa yaliyoitishwa na Sall, ambayo yalipendekeza uchaguzi huo ufanyike mwezi Juni.


Bar aza pia lilitoa orodha ya wagombea 19 waliopendekezwa mnamo Januari kushiriki katika uchaguzi wa urais.


Sall alisema mwezi uliopita kwamba atajiuzulu muda wake kama rais utakapokamilika Aprili 2.


Rais, ambaye amekuwa madarakani tangu 2012, alitangaza kusimamisha kwa muda usiojulikana uchaguzi wa rais wa Februari 25 akitaja mzozo kuhusu orodha ya wagombea na madai ya ufisadi wa majaji wa kikatiba, na kusababisha machafuko ya kisiasa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso