DAR, DOM, MWANZA NA ARUSHA KUFUNGIWA KAMERA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday 12 March 2024

DAR, DOM, MWANZA NA ARUSHA KUFUNGIWA KAMERA

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Hamad Masauni amekutana na Kikosikazi cha Miji Salama kinachoratibu na kusimamia utekelezaji wa mradi wa ufungaji wa kamera za kuzuia uhalifu.



Kamera hizo awali zitafungwa katika majiji matano ili kudhibiti matukio ya uhalifu ukiwemo ujambazi, ukiukwaji wa sheria za usalama barabarani, wizi na matukio mengine ya kiuhalifu.


Majiji yatakayofungwa kamera hizo ni Dodoma, Dar es Salaam, Mwanza na Arusha huku lengo likiwa ni kufunga kamera hizo katika mikoa yote nchini kwa siku zijazo. Masauni alisema kuna maeneo ambayo yanatakiwa yawe na udhibiti wa uhalifu hasa kwa kutumia teknolojia na baadhi ya nchi tayari wana mfumo huo na wameanza kufanikiwa kudhibiti uhalifu na makosa ya ukiukwaji wa sheria za usalama.


“Serikali tumeanza jitihada za kufunga kamera, sasa mkiwa wajumbe wa kikosi kazi mfahamu mna jukumu kubwa kwa nchi kuhakikisha mradi huu unatekelezeka ili uwe na manufaa kwa nchi yetu,” alisema. Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini, Camilius Wambura aliagiza wajumbe wa kikosikazi hicho wahakikishe wanaupitia mkataba huo wa ufungaji wa kamera hizo.

  • habarileo_tz's profile picture

    DAR ES SALAAM: Rais Samia Suluhu Hassan amepangua safu ya Wakuu wa Mikoa, Wakuu wa Wilaya, Wakurugenzi wa Wilaya na Makatibu Tawala wa wilaya baada ya kuteua tisa na kuhamisha watatu usiku wa kuamkia leo, Machi 12.


    Miongoni mwa teuzi mpya ni aliyekuwa Naibu Katibu Mkuu CCM, Anamringa Macha ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga. Macha anachukua nafasi ya Christina Mndeme ambaye pia amewahi kuwa Naibu Katibu Mkuu CCM Bara na sasa anateuliwa kuwa Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).

    Uteuzi huu umekuja siku tatu tangu kiongozi huyo wa nchi apangue safu za uongozi katika ngazi ya mikoa na wilaya.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso