CHAWA WA MAMA MARUFUKU WANASAKA MADARAKA TU-CCM - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 7 August 2023

CHAWA WA MAMA MARUFUKU WANASAKA MADARAKA TU-CCM

Chama cha Mapinduzi (CCM) kimepiga marufuku kundi la ‘chama wa mama’ kikieleza dhamira yao ni kusaka madaraka tu.

Katibu wa CCM Wilaya ya Ilala Frata Katumwa


Chama hicho pia kimetoa maelekezo ya kubadilishwa jina kutoka ‘chawa wa mama’ na kuwa ‘watetezi wa mama’ ambao watakuwa wamejitambulisha kutoka nje ya chama na siyo waliopo ndani ya jumuiya tatu za CCM zinazotumia majukwaa yake kumsaidia Rais Samia Suluhu Hassan.


Katibu wa chama hicho Wilaya ya Ilala, Frata Katumwa akizungumza na wajumbe wa baraza la wilaya hiyo la Umoja wa Wanawake wa CCM (UWT) wiki mbili zilizopita, alisema uamuzi huo ni maelekezo ya Halmashauri Kuu ya chama hicho iliyokutana Julai 9, mwaka huu.


“Kuna maagizo maalumu ambayo sitakosa kuyaeleza katika hili baraza na nina uhakika mtendaji wa UWT utakuwa umeshapokea maelekezo hayo kutoka Halmashauri Kuu ya Taifa ya chama, kikao kilichofanyika juzi (Julai 9, 2023), kuna kikundi kimeibuka kinajiita chawa wa mama,” alisema Frata katika video inayosambaa mtandaoni.


“Huwezi kuanzisha chama ndani ya chama, wanajivisha kivuli cha chawa wa mama, lakini malengo yao ni kutafuta uongozi, kuunda makundi ndani ya chama ili kutafuta nafasi, hili haliwezekani. Kama wanataka chawa wanashauri jina libadilike kuwa mtetezi wa mama. Lakini wafuate taratibu, sasa kinachoshangaza UWT, UVCCM, JWT wana msemo wa chawa wa mama. Sasa ukiwa chawa wa mama ndiyo utamsemea vizuri? Tunachojichanganya ni nini?” alihoji Frata.


Juhudi za kupata uongozi wa juu wa CCM kuzungumzia suala hilo ziligonga mwamba, baada ya simu ya msemaji wa chama hicho, Sophia Mjema kutopatikana, huku Katibu Mkuu, Daniel Chongolo akiwa kwenye kikao kwa mujibu wa taarifa za msaidizi wake aliyepokea simu.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso