WATU 16 WAFARIKI DUNIA KWA AJALI YA BASI KULIGONGA LORI LILILOPAKIWA 12 WAKIPOTEZA MAISHA PAPO HAPO - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 6 January 2023

WATU 16 WAFARIKI DUNIA KWA AJALI YA BASI KULIGONGA LORI LILILOPAKIWA 12 WAKIPOTEZA MAISHA PAPO HAPO

Picha hii sio halisia na picha za ajali yenyewe nchini Uganda

Takriban watu 16 wameuawa wakati basi la abiria lilipogonga lori moja Ijumaa asubuhi kwenye barabara kuu ya Uganda inayounganisha mji mkuu, Kampala, na mji wa kaskazini wa Gulu.


Polisi wanasema watu 12 walifariki papo hapo huku wengine wanne wakifariki baadaye hospitalini na Wasafiri wengine kadhaa kwenye basi hilo walijeruhiwa.


Lori hilo lilisemekana kuegeshwa na kupakia mizigo takriban kilomita moja kutoka Kamdini Corner kituo maarufu cha kusimama na ukaguzi kaskazini mwa nchi.


Kumekuwa na viwango vya kutisha vya ajali za barabarani nchini katika wiki za hivi karibuni na haswa katika msimu wa sikukuu na Ripoti ya polisi wa trafiki mapema wiki hii ilifichua kuwa ajali 104 za barabarani zilirekodiwa kati ya 30 Desemba na 1 Januari.


Takriban watu 35 waliuawa katika ajali hizo za barabara pekee huku Ajali za barabarani zinatajwa kuwa janga la muda mrefu nchini humo. 


Polisi wa trafiki walisajili zaidi ya ajali 4,000 kote nchini Uganda mnamo 2021, nyingi zikiwa mbaya.


chanzo:BBC

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso