UKAME CHANZO CHA KUKATIKA KWA UMEME NCHINI TANESCO YAFUNGUKA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 31 October 2022

UKAME CHANZO CHA KUKATIKA KWA UMEME NCHINI TANESCO YAFUNGUKA



Shirika la Umeme (Tanesco) limesema ukame unaoikabili nchi ndiyo sababu kubwa ya changamoto ya ukatikaji wa umeme wa mara kwa mara unaoendelea nchini.


Hayo yameelezwa jana Oktoba 30 na Kaimu Mkurugenzi wa Huduma kwa Wateja wa Shirika hilo, Martin Mwambene.


Mwambene amesema mabwawa ya kuzalisha umeme ya Hale, Kihansi, Nyumba ya Mungu na Pangani yenye uwezo wa kuzalisha megawati 266 za umeme sasa yanazalisha megawati 34 tu.


Ameitaja iliyoathirika kwa kiasi kikubwa kutokana uzalishaji mdogo kuwa pamoja na Arusha, Kilimanjaro na Tanga.


“Kutokana na ukame huu mkubwa, mikoa hiyo inalazimika kupata umeme wake kutoka katika vituo vya kuzalisha umeme kwa kutumia gesi asilia vilivyopo Dar es Salaam,” amesema.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso