MUME NA MKE WAKUTANA MSIBANI, MWANAUME AMUUA MKE WAKE-GEITA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 3 August 2022

MUME NA MKE WAKUTANA MSIBANI, MWANAUME AMUUA MKE WAKE-GEITA



Mariam Masanja 22, mkazi wa Kijiji cha Nyabugela, Kata ya Mganza wilayani Chato mkoani Geita, ameuawa kwa kupigwa na kitu kizito kichwani na kung'atwa kidevu na mme wake Edward Franscis 20, ambao walikutana kwenye familia ya mwanamke kuhani msiba baada ya ugomvi wao wa muda mrefu.


Wawili hao walikutana kwenye msiba wa kaka wa marehemu ambapo marehemu alikuwa mkoani Mwanza kwa dada yake baada ya kugombana na mme wake ndipo aliporudi kwao baada ya kusikia kaka yake amefariki.


Wazazi wa marehemu wameeleza walivyopata taarifa za mtoto wao kuuawa na mme wake huku baba mzazi wa marehemu anasema wawili hao walikuwa na ugomvi wa mara kwa mara wa wivu wa kimapenzi.


Mwenyekiti wa Kijiji cha Nyabugela Metusela Mgema, amesema wawili hao walifika mara kadhaa kwenye ofisi yake kwa ajili ya migogoro ndani ya familia yao ambayo ilikuwa inasuruhishwa mara kwa mara lakini mpaka kufikia kifo cha mwanamke wawili hao walikuwa wameachana.

chanzo:EATV

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso