TETESI ZA USAJILI DECEMBER 28 - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday 28 December 2021

TETESI ZA USAJILI DECEMBER 28

 

th

CHANZO CHA PICHA,

Tottenham wanaongoza katika kinyang'anyiro cha kumsajili kiungo wa kati wa Ivory Coast Franck Kessie, ambaye mkataba wake na AC Milan unakamilika msimu wa joto. Arsenal na Manchester United pia wanamtaka mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 lakini Spurs tayari wamefanya mazungumzo na kambi ya Kessie. (Express)

Mkufunzi wa Newcastle United Eddie Howe hataki kumnunua kiungo wa kati wa Tottenham Muingereza Dele Alli mwenye umri wa miaka 25 kwa vile anataka kuimarisha sehemu nyingine za timu yake mwezi Januari. (Football Insider)

th

CHANZO CHA PICHA,

Chelsea wako tayari kushindana na Liverpool kujaribu kumsajili winga wa Brazil Raphinha, 25, kutoka Leeds United msimu wa joto. (Sport Italia, via Express)

Real Madrid wanavutiwa na beki wa kulia wa Chelsea na England Reece James, 22, na wanaweza kujaribu kuwajaribu The Blues kwa kumpa winga wa Ubelgiji Eden Hazard kama sehemu ya mkataba wowote. (El Nacional - in Catalan)

Kipaumbele cha Real Madrid ni kumsajili mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland, 21, kutoka Borussia Dortmund msimu ujao lakini klabu hiyo ya Uhispania inamtazama mshambuliaji wa Fiorentina mwenye umri wa miaka 21 na Serbia Dusan Vlahovic kama mbadala wake iwapo watamkosa. (El Nacional - in Catalan)

Winga wa Chelsea na Uingereza Callum Hudson-Odoi, 21, analengwa na Napoli, ambayo inanolewa na mkufunzi wa zamani wa Blues Maurizio Sarri. (Tuttosport, via Football Italia)

TH

CHANZO CHA PICHA,

Barcelona wanataka kumuachilia huru mchezaji wa Brazil Philippe Coutinho na chaguo analopendelea mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 ni kwenda Arsenal. (Sport - in Spanish)

Klabu ya Ufaransa Lille inataka angalau euro 30m (£25m) ikiwa watalazimika kumuuza mlinzi wa Uholanzi Sven Botman, 21. (Tuttomercatoweb - in Italian)

Mshambulizi wa Italia Andrea Belotti yuko tayari kuondoka Torino wakati mkataba wake na timu hiyo ya Serie A utakapokamilika msimu wa joto, huku AC Milan, Napoli na Fiorentina zikimwania mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28. (Calciomercato, via Football Italia)

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso