CHADEMA KANDA YA SERENGETI YAZINDUA MATAWI MAPYA KAHAMA, YATAKA USHIRIKIANO NA UMOJA KWA WANACHAMA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Sunday, 17 May 2026

CHADEMA KANDA YA SERENGETI YAZINDUA MATAWI MAPYA KAHAMA, YATAKA USHIRIKIANO NA UMOJA KWA WANACHAMA


Makamu mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar Said Mzee (kushoto), akipandisha bendera ya chama hicho kuashiria uzinduzi rasmi wa tawi la Chama hicho, katika kata ya Nyahanga wilayani Kahama mkoani Shinyanga, kwa lengo la kusogeza huduma za kichama kwa wananchi, kurahisisha utatuzi wa kero zao.

Na Neema Nkumbi, Kahama

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Kanda ya Serengeti, kimezindua matawi mapya 20 ya chama hicho katika kata tano za jimbo la Kahama Mjini, mkoani Shinyanga.


Katibu wa Chadema wilaya ya Kahama (Msalala, Kahama Mjini na Ushetu) Samuel Peter amesema uzinduzi wa matawi hayo unalenga kurejesha shughuli za kichama, kusogeza huduma za chama kwa wananchi na kurejesha uhai wa chama hicho katika ngazi za chini.


Peter amewataka wanachama wa chama hicho pamoja na wananchi kwa ujumla kuyatumia matawi hayo kuwasilisha kero na changamoto zao ili zitafutiwe ufumbuzi wa haraka.


Amewahimiza viongozi wa matawi kushirikiana na wananchi kuendelea kudumisha umoja, mshikamano na ushirikiano ndani ya chama, na kusisitiza umuhimu wa kushiriki kikamilifu katika shughuli za chama kuanzia ngazi ya tawi hadi Taifa.


Matawi hayo yamezinduliwa rasmi katika kata ya Mhongolo, Kahama Mjini, Majengo, Zongomela na Nyahanga.


"Leo tulikuwa na operesheni ya maandalizi ya mkutano mkubwa na wa kihistoria hapa Kahama utakaofanyika hapo kesho kwenye viwanja vya Fantom, Manispaa ya Kahama." Amesema na kuongeza


"Wananchi wote tunawaalika kuhudhuria mkutano huu, viongozi wa kitaifa wa Chama watakuwepo, sio mkutano wa kukosa kabisa."



No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso