UBELGIJI, URENO ZAPANDA VIWANGO VYA FIFA UINGEREZA NA UHOLANZI WASHUKA. - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 4 April 2024

UBELGIJI, URENO ZAPANDA VIWANGO VYA FIFA UINGEREZA NA UHOLANZI WASHUKA.

 




Shirikisho la mpira wa miguu Duniani (FIFA) limetoa orodha ya timu 10 za mataifa amblimbali zilizo katika viwango bora.


Katika orodha hiyo mabingwa wa kombe la Dunia mwaka 2022 Argentina wamebaki nafasi yao ya kwanza, Ufaransa waliomaliza nafasi ya pili kombe la Dunia mwaka 2022 wamefanikiwa kubaki nafasi ya pili.


Ubelgiji amepanda kwa nafasi moja kutoka nafasi ya nne hadi ya tatu wakati huo Uingereza wameshuka kwa nafasi moja kutoka nafasi ya tatu hadi nafasi ya nne sanjali na hayo Brazil wamebaki nafasi ya tano.


Kwingineko Ureno kapanda kwa nafasi moja kutoka nafasi ya saba hadi nafasi ya sita akimshusha Uholanzi aliyeangukia nafasi ya saba.


Hispania kabaki nafasi yake ya nane, Italia kabaki nafasi ya tisa na Crotia wao wakibaki nafasi ya 10 palepale.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso