MLIPUKO WA GESI UMETOKEA MJI MKUU WA KENYA NAIROBI NA KUUA WATU WATATU NA WENGINE 300 KUJERUHIWA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Saturday 3 February 2024

MLIPUKO WA GESI UMETOKEA MJI MKUU WA KENYA NAIROBI NA KUUA WATU WATATU NA WENGINE 300 KUJERUHIWA

Lori lililokuwa limebeba mitungi ya gesi lililipuka katika wilaya ya Embakasi mwendo wa 23:30 (20:30 GMT), "na kuwasha moto mkubwa" msemaji wa serikali alisema.




Nyumba  biashara na magari viliharibiwa huku video ikionyesha moto mkubwa ukiwaka karibu na majengo ya ghorofa. Hapo awali  serikali  imesema mlipuko huo umetokea katika kiwanda cha gesi   chanzo  cha moto huo  bado  hakijajulikana.


 

Msemaji wa serikali Isaac Mwaura amesema eneo la mlipuko kwa  sasa limezingirwa na kituo cha kuendesha operesheni ya uokoaji kimeanzishwa kusaidia kuratibu shughuli za uokoaji.

 

"Wakenya wameshauriwa kuepuka eneo lililozingirwa ili kuruhusu shughuli ya uokoaji kutekelezwa  bila  usumbufu "amesema  msemaji wa serikali

 

Moto huo unaripotiwa kuenea katika majengo kadhaa ya ghorofa na kusababisha hofu kutanda  kwa wananchi wa eneo hilo  na idadi ya waliojeruhiwa inaweza kuongezeka zaidi.

 

Mmoja wa waliojeruhiwa  Boniface Sifuna  ameelezeea kilichotokea kwa shirika la habari la Reuters: "Nilichomwa na mtungi wa gesi uliolipuka nilipokuwa nikijaribu kujiokoa " alisema

 

Shahidi ambaye jina lake halikutajwa amesema  "milipuko mikubwa, mipira mikubwa ya moto, watu kupiga mayowe na kukimbia kila mahali kwa kuhofia milipuko zaidi".

 

Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya limesema kwenye mitandao ya kijamii kwamba wafanyakazi wamekuwa "wakipambana na moto huo bila kuchoka".

 

    Chanzo: BBC SWAHILI                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                                             

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso