TEGEMEO MCHIMBA MADINI GEITA AUAWA KWA KUKATWA SHINGONI - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Sunday 6 November 2022

TEGEMEO MCHIMBA MADINI GEITA AUAWA KWA KUKATWA SHINGONI


Mchimbaji mdogo wa dhahabu, Tegemeo Msure (38), mkazi wa kijiji cha Ihanga kilichopo kata ya Buziku, wilaya ya Chato, mkoani Geita ameuawa kwa kukatwa na kitu chenye ncha kali shingoni na kichwani.


Kamanda wa polisi mkoa wa Geita, Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema limetokea Novemba 2, 2022 na kwamba kabla ya kuuawa, wauaji walitumia bunduki ya AK47 kumtisha ili asimame akiwa kwenye pikipiki yake.


Anasema baada ya kutishwa, alisimama na walimkamata wakamfunga kwa kamba ya katani shingoni na kumzungushia tumboni na mikononi na kumburuza hadi umbali wa mita 170 toka eneo aliposimamishwa na kufanikisha azma yao ya mauaji kwa kumkatakata mapanga,” amesema Jongo.


Kamanda ameeleza wakati wakitekeleza mauaji hayo alitokea msamaria mwema akitaka kumuokoa marehemu lakini wauaji walifyatua risasi hewani ili kumtisha ashindwe kutoa msaada.
Amesema kwenye eneo la tukio limeokotwa ganda la risasi moja inayotumika kwenye silaha ya AK47.


Kufuatia tukio hilo, kikosi cha kupambana na ujambazi kimefanikiwa kuwakamata watuhumiwa wanne ambapo watatu ni Watanzania na mmoja ni raia wa Burundi anayedaiwa kuingia nchini na silaha hiyo ambayo haina usajili.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso