MABASI YAENDAYO MIKOANI TOKA DAR YARUHUSIWA KUINGIA KWENYE STENDI BINAFSI - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Friday 2 September 2022

MABASI YAENDAYO MIKOANI TOKA DAR YARUHUSIWA KUINGIA KWENYE STENDI BINAFSI

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla ametangaza kuondoa katazo lililokuwa likizuia Mabasi yaendayo mikoani na nje ya Nchi kutoruhusiwa kupakia abiria au kushusha katika Vituo binafsi na badala yake ameruhusu utaratibu huo kuendelea kwa sharti la kila basi kuingia ndani ya Kituo kikuu cha Mabasi cha Magufuli.


Na  James lyatuu, Dar es salaam

RC Makalla ametoa maamuzi hayo wakati wa kikao cha pamoja baina ya LATRA, Wamiliki wa Stendi binafsi na Halmashauri ya Ubungo na kubaini pasipokuwa na shaka kuwa waliotengeneza Vituo binafsi walifuata taratibu na kupatiwa vibali na LATRA baada ya kukidhi vigezo.


Miongoni mwa vigezo vilivyotolewa na LATRA ili kuruhusiwa kuanzisha Stendi binafsi ni pamoja na uwepo wa Vyoo, Sehemu ya mapumzimo kwa abiria, viburudisho na sehemu ya maegesho.


Kutokana na  Makalla ameridhia Vituo binafsi 5 vilivyohakikiwa kuendelea kutoa huduma na kufungua milango kwa wamiliki wengine wanaohitaji kuwa na Vituo binafsi kushirikiana na LATRA ili wapatiwe vigezo vinavyohitajika ambapo wamepewa Mamlaka ya kufuta au kutoa leseni.


Aidha Makalla ameagiza Halmashauri ya Manispaa ya Ubungo kukaa kikao mara moja na wamiliki wa Stendi binafsi ili kuona njia bora ya ukusanyaji wa mapato.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso