MTANZANIA ADAKWA AKIWA NA WAHAMIAJI HARAMU - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Thursday 11 August 2022

MTANZANIA ADAKWA AKIWA NA WAHAMIAJI HARAMU




Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na Jeshi la uhamiaji mkoani Kilimanjaro wamefanikiwa kuwakamata wahamiaji haramu 47 raia wa Ethiopia walioingia nchini kwa njia za panya katika eneo la Mgagao wilayani Mwanga.


Akizungumza na waandishi wa habari leo Agosti 11, Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji Mkoa wa Kilimanjaro, Edward Mwenda amesema wahamiaji hao wamekamatwa usiku wa kuamkia leo katika operesheni maalumu inayoendelea mkoani humo.


"Katika operesheni maalum ambayo imefanyika katika mkoa wetu usiku wa kuamkia leo tumewakamata raia wa Ethiopia 47, akiwemo msafarishaji mmoja wa Tanzania ambaye tunamshikilia kwa mahojiano zaidi.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso