Serikali yatangaza ajira 17,412 leo - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Wednesday 20 April 2022

Serikali yatangaza ajira 17,412 leo

 WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OR-TAMISEMI), Bw. Innocent Bashungwa amesema kuwa katika mwaka huu wa fedha 2021/22 Serikali inatarajia kuajiri watumishi 17,412 ambapo nafasi 9,800 ni za walimu na 7,612 ni za kada za afya.


Ameyasema hayo leo Aprili 20,2022 wakati akitoa maelezo kuhusu hoja za wabunge zilizojitokeza wakati wa kujadili hotuba ya bajeti ya Ofisi ya OR-TAMISEMI kwa mwaka wa fedha 2022/2023 bungeni jijini Dodoma.

Makadirio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2022/23 kwa OR-TAMISEMI ni Shilingi Trilioni 8.8 kwa ajili ya Ofisi ya Rais-TAMISEMI Fungu 56, Tume ya Utumishi wa Walimu Fungu Na. 2 na Mafungu 26 ya mikoa yanayojumuisha halmashauri 184.

"Mheshimiwa Spika, nachukua fursa hii kwa kumshukuru Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kutoa idhini ya ajira za watumishi wa Sekta ya Elimu na Afya 17,412 ambapo nafasi 9,800 ni za walimu na 7,612 ni za kada za afya ambao wataajiriwa katika mwaka huu wa Fedha 2021/22.

"Naomba kutoa taarifa rasmi kuwa Watanzania wenye sifa wanaelekezwa kuanza kuomba kuanzia leo. Aidha, napenda kuwaelekeza kuwa maombi ya ajira hizi ni bure na yanafanyika kupitia mfumo wa kielektroniki ambao maelekezo yake yatakuwa katika tangazo la ajira.Asilimia tatu ya ajira hizo ni kuajiri watu wenye ulemavu kulingana na sheria,"amesema Mheshimiwa Bashungwa.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso