UZALENDO WA KWELI HUPIMWA KWA VITENDO VYA KULINDA TAIFA - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Tuesday, 23 December 2025

UZALENDO WA KWELI HUPIMWA KWA VITENDO VYA KULINDA TAIFA




Vijana wamehimizwa kutambua kuwa mzalendo wa kweli hupimwa kwa vitendo vya kulinda taifa.


Jackline Mwafongo, mkazi wa Mbeya, ameeleza kuwa vurugu huleta hofu na uharibifu wa mali, jambo ambalo huathiri moja kwa moja ustawi wa vijana na sekta binafsi.


Badala ya kujihusisha na miito ya uasi, wananchi wameaswa kuiga mifano ya ubunifu kama ule wa kukodisha power bank uliozinduliwa na kijana Thomas Ryoba, ambao unalenga kutatua changamoto za jamii na kuongeza kipato.


Jackline amesema hayo wakati Jeshi la Polisi likitoa taarifa ya kuimarika kwa usalama kuelekea sikukuu za mwisho wa mwaka,ambnapo limewataka vijana na raia nchini kupuuza taarifa za uchochezi zinazotoka nje ya nchi na kujikita na maisha yenye tija.


Wananchi wameonya kuwa taarifa nyingi mtandaoni zinalenga kupandikiza mgawanyiko na kudhoofisha uchumi wa taifa kupitia maandamano na vurugu ambazo hazizingatii historia na utulivu wa Tanzania wa zaidi ya miaka 60.


Maoni ya wananchi yamesisitiza kuwa sauti ya utulivu imeshinda kelele za chuki, na kutoa wito kwa kila mmoja kutambua thamani ya amani kama nyenzo kuu ya kufanya shughuli halali.


Aidha, msisitizo umetolewa kuwa usalama wa mali na miundombinu ya biashara ni jukumu la pamoja, kwani uharibifu wowote unarudisha nyuma jitihada za serikali za kukuza uchumi jumuishi. Kupitia kampeni ya "Nchi Kwanza," vijana wametakiwa kuendelea kuwa nguzo ya amani ili kuhakikisha uwekezaji na ajira nchini vinazidi kuongezeka bila bughudha.

No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso