SILAHA MPYA YA ANGA YA NYUKILIA TOKA URUSI INATIA WASIWASI DUNIA. - HUHESO DIGITAL BLOG

Breaking

Post Top Ad

Monday 19 February 2024

SILAHA MPYA YA ANGA YA NYUKILIA TOKA URUSI INATIA WASIWASI DUNIA.


Marekani imesema ina wasiwasi kuwa Urusi imetengeneza silaha mpya inayoweza kushambulia satelaiti.



Lakini Urusi imekanusha madai hayo ya Marekani, ikisema ni njama ya kutoa shutuma ili kulilazimisha Bunge la Marekani kutoa fedha za ziada kwa ajili ya Ukraine.


Katika mitandao ya habari ya New York Times, ABC na CBS - ripoti zilisema tishio hilo lilitokana na silaha za nyuklia zilizotengenezwa na Urusi. Kuna hofu kuwa zinaweza kutumika kushambulia satelaiti za Marekani angani.


Akizungumza na waaandishi wa habari hivi karibuni kuhusu silaha hii, msemaji wa usalama wa taifa katika Ikulu ya Marekani John Kirby, alisema hakuna tishio la moja kwa moja kwa watu wa Marekani.


John Kirby, amesema Rais Joe Biden amefahamishwa kuhusu suala hilo, alisema utawala wa Biden umelichukulia suala hilo 'kwa uzito mkubwa'.


Kadhalika alisema, Rais Biden ameamuru mawasiliano ya moja kwa moja ya kidiplomasia na Urusi juu ya suala hili.


John Kirby aliwaambia wanahabari hakuna ushahidi kwamba silaha hiyo imetumiwa.


Mbali na maoni ya John Kirby, maafisa wa serikali ya Marekani bado hawajatoa taarifa zozote kuhusu tishio hilo.

Mshauri wa Usalama wa Taifa, Jake Sullivan amedokeza kuwa serikali ya Marekani imekuwa kimya kwa makusudi.


Pia aliwaambia waandishi wa habari kwamba mashirika ya kijasusi ya Marekani yatafanya kazi kukusanya taarifa kuhusu tishio hilo.


No comments:

Post a Comment

Post Top Ad

Pages

Huheso